Monday, November 15, 2010

Na Herman
MAJAJI wa Shindano la Bongo Star Search (BSS) linalorushwa hewani kupitia Televisheni ya ITV, Salama Jabir na Joachim Kimaryo a.k.a Master J hivi karibuni walijikuta wakitibuana na kufikia hatua ya kurushiana maneno makali, Ijumaa Wikienda lilishuhudia.

Tukio hilo, lilitokea juzikati maeneo ya Posta, jijini Dar es Salaam ndani ya Ukumbi wa Water Front wakati mastaa wa shindano hilo wakiwa katika mchakato wa kuandaa kipindi cha shindano hilo.

Wakiwa katika zoezi hilo, mara kadhaa Master J ambaye ni ‘prodyuza’ kitaaluma alikuwa akiwaambia washiriki kutojali sana namna wanavyokosolewa na Salama huku akidai kuwa jaji mwenzake huyo, siku hiyo alikuwa ameamka vibaya.
Master J.
Baada ya Salama kusikia maneno hayo, alimtolea uvivu Master J huku akikanusha sentensi ya kuamka vibaya na kueleza kwamba anavyokosoa si kutokana na madai hayo, bali anachokizungumza ndiyo ukweli wa mambo.

Licha ya Salama ‘kufyumu’ na kutoa maneno hayo, Master J aliendelea kusisitiza kauli yake hali iliyowafanya wawili hao kutibuana kwa muda.

Katika mtibuano huo, Salama alifikia hatua ya kumchambua Master J kinagaubaga huku akieleza kuwa, hawezi kuamka vibaya kwa kuwa kitanda anacholalia yeye ni kizuri kuliko kile kinacholaliwa na prodyuza huyo.

Hata hivyo, Jaji Mkuu wa Shindano hilo, Ritta Paulsen ‘Madam Ritta’ aliamua kuingilia kati mzozo huo na kuupotezea.
Salama Jabir.
Tags: herman mwampyate

No comments:

Post a Comment