Monday, November 1, 2010

Maziwa ya NAN 2 sasa yarudi sokoni


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Maziwa ya watoto aina ya NaN 2 yaliyokua yamezuiwa kuuzwa nchini yamepewa kibali maalum kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania baada ya kukaguliwa na kuhakikiwa ubora wake.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja Maendeleo na Biashara wa Nestle Tanzania Bw. Faiz Rasool ambao ndio wasambazaji wakuu wa maziwa hayo nchini amesema kwamb, baada ya kufikia makubaliano na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) sasa wameyarudisha tena sokoni.

Mnamo Oktoba 8 mwaka huu mamlaka ya chakula na dawa yalisimamisha kwa muda kuingiza, kusambaza na uuzwaji wa maziwa hayo ya NAN2 baada ya kudai kwamba hayana viwango vinavyomfaa mlaji.

Kwa mujibu wa Meneja huyo maziwa ya NAN 2 yanatengeezwa nchini Ufaransa chini ya Nestle na yamesajiliwa kwa namba SAS F-77446 yakiwa yamewekewa nembo ya Kiswahili na Kiingereza.

Aidha katika kuyatofautisha maziwa hayo halisi nay ale yanayuodaiwa kuwa ni feki Meneja huyo amesema kwamba nembo ya NAN 2 ipo kwa rangi ya bluu na katika lebo hiyo kuna picha picha ya ndege weupe watatu ikiwa ni sehemu ya nembo ya Nestle.

Katika taarifa ya TFDA imewatahadharisha wananchi kwamba wanatakiwa kutumia maziwa ya watoto yaliyosajiliwa na Nestle ambayo ni Lactogen1, Lactogen 2, NAN1 na NAN2.

Agosti 13 mwaka huu Mamlaka hiyo ilisema inachunguza maziwa ya aina ya NAN 2 kutoka a na kudaiwa kutokidhi vigezo, imeelezwa aidha mamlaka hiyo imesimamisha kwa muda uingizaji maziwa hayo kutoka nje hadi uchunguzi utakapokamilika.

No comments:

Post a Comment