Tuesday, November 2, 2010

KIBAKA AKAMATWA AKIIBA DUKANI MORO

Kibaka akiwa amenyanyuliwa mtindo wa "Tanganyika Jack" na askari.
KIJANA mmoja anayesadikiwa kuwa ni kibaka jana mchana,alinaswa maeneo ya Mwembesongo mjini Morogoro akiiba nguo ndani ya duka linalojulikama kama Arawa.

Habari zilizopatikana eneo la tukio zilidai kwamba kibaka aliyefika dukani hapo akiwa na mwenzake ambaye alifanikiwa kukimbia, waliiba suruali mbili na magauni matatu.

"Huyu kibaka alifika hapa na mwenzake ambaye alikuwa akinisemesha mambo ya uchaguzi mkuu. Wakati huo huyu kibaka tuliyemkamata alikuwa akijifanya kuchagua nguo na baada ya muda nilimwona akiweka suruali ya "Jeans" na gauni kwenye mfuko ambao walikuja nao.

Kuona hivyo nilitoka nje fasta; yule aliyekuwa akinisemesha alifanikiwa kukimbia na huyu niliamua kumfungia kwenye haya mageti ya chuma," alisema muuza duka hilo aliyejitambulisha kwa jina la Focus Riwa.

Mtandao huu ulishuhudia kundi la wananchi, baadhi yao wakiwa na mawe na magongo, wakimtaka mwenye duka hilo kumtoa nje kibaka huyo "wamshikishe adabu".

Hata hivyo, baada ya kuona umati huo, mmiliki wa duka hilo aligoma kumtoa nje kibaka huyo na badala yake alitoa taarifa polisi ambao muda mfupi walifika na kumchukua kibaka huyo.
Wananchi wakimsuburi kibaka nje ya Arawa Shop.
Askari na wananchi wakisaidiana kumtoa kibaka nje ya Arawa Shop.
Mtuhumiwa akiswekwa katika karandinga la polisi.
Askari wakiondoka na mtuhumiwa kwenda "kwa Pilato".

No comments:

Post a Comment