Tuesday, November 2, 2010

GARI LAINGIA CHUMBANI HUKO AUSTRALIA

Gari lililovamia chumba jijini Melbourne, Australia.
GARI ndogo liligonga ukuta wa nyumba moja na kujikuta limeishia katika chumba cha kulala cha nyumba moja jijini Melbourne, Australia, ambapo mwenye chumba alinusurika kwani alikuwa katika chumba kingine akitumia kompyuta yake.

Mwenye chumba hicho, Demitrios Bisbelis, ashukuru hali iliyomfanya akose usingizi ambapo aliamua kuondoka chumbani kwake kwenda kutazama Internet kwenye kompyuta.

"Kitanda changu kimevunjwavunjwa kabisa. Nina uhakika nisingesalimika iwapo ningekuwa kitandani wakati huo," alisema baada ya tukio hilo.

Kwa mujibu wa polisi, gari hilo liliruka juu na kuishia kukivunjilia mbali chumba cha Bisbelis baada ya kugonga ukingo wa barabara.

Dreva na abiria katika gari hilo walinusurika kwa majeraha kidogo na wamefikishwa polisi kuhusiana na tukio hilo.
Sura nyingine ya ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment