Tuesday, November 2, 2010

DK SHEIN ATANGAZWA RAIS ZANZIBAR!

Tume ya Uchaguzi ya Taifa imemtangaza sasa hivi Dk. Mohamed Shein wa CCM kuwa Rais wa Zanzibar baada ya kupata jumla ya kura 179,809 sawa na 50.1% dhidi ya maalim Seif wa Cuf. Maalim Seif ameyakubali matokeo na amempongezi kwa dhati kabisa Dk. shein kwa kupata ridhaa ya Wazanibari ya kuwaongoza kwa miaka 5. "Najua kabisa dk. Mohamed Shein ana uwezo na mahaba ya dhadi ya kuongoza na kuiunganisha nchi yetu", alisema Maalim Seif na kushangiliwa kwa makofi. Kwa maana hiyo Maalim Seif atakuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi kwa mujibu wa muafaka.

No comments:

Post a Comment