Thursday, February 16, 2012

Ngurdoto Museums at Arusha National Park

                                                               Hili ni fuvu la kiboko

                                                                      Bundi

                                                                    fuvu la faru
                                                          Picha ya mlima ulivyo
                                                           Njia za kufika mlima meru
                                                              vipepeo
                                                                         ndege
                                                                       njiwa ama kizungu pigeon
                                                                    panya buku











                                      panya buku wanatumika sana kwenye uteguzi wa mabomu

Monday, February 13, 2012

RAIS KIKWETE AONGOZA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA CCM MJINI DODOMA JANA

 

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete (wa tatu kulia) akiwa meza kuu na Rais wa Zanzibar Dkt Mohamed Shein (wa pili kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM (Visiwani) na Rais Mstaafu  wa Zanzibar Dkt Amani Abeid Karume (wa tatu kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (wa kwanza kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mh Pius Msekwa (wa kwanza kulia) na Katibu Mkuu wa CCM Mh Wilson Mkama (wa pili kulia) kabla ya kuanza kwa mkutano wa Halmashauri Kuu jana katika jengo la White House la Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma.…

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete (wa tatu kulia) akiwa meza kuu na Rais wa Zanzibar Dkt Mohamed Shein (wa pili kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM (Visiwani) na Rais Mstaafu  wa Zanzibar Dkt Amani Abeid Karume (wa tatu kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (wa kwanza kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mh Pius Msekwa (wa kwanza kulia) na Katibu Mkuu wa CCM Mh Wilson Mkama (wa pili kulia) kabla ya kuanza kwa mkutano wa Halmashauri Kuu jana katika jengo la White House la Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM katika mkutano huo jana.
 
 PICHA ZOTE NA HERMAN

Chipolopolo oyeeeee

Hatimaye siku ya jana ilikuwa ni siku nzuri sana kwa timu ya zambia a.k.a wana chipolopolo kuweza kutwaa kombe lao na kudedicate ushindi huo kwa kuwakumbuka wenzao walipata ajali huko gabon.

Tuesday, November 16, 2010

Neno La Leo: Msijiulize, Nani Atakuwa Rais 2015, Jiulizeni, Mtapataje?

Ndugu zangu,
KATIKA kuadhimisha miaka kumi ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi, CCM na miaka 20 ya Azimio la Arusha, Mwalimu Julius Nyerere alikubali kufanya mahojiano ya kipekee na ya aina yake na Mhariri wa gazeti la Uhuru. Huo ulikuwa ni mwaka 1987.

Katika mahojiano yale Mwalimu, akiwa Mwenyekiti wa CCM hakusita kutamka bayana, kuwa Chama alichokuwa akikiongoza kilikuwa na kasoro na mapungufu mengi.

Mwalimu aliona dalili za kupungua kwa moyo wa kujitolea. Aliona dalili za kupungua kwa maadili ya uongozi. Mwalimu aliona dalili za mioyo ya kimamluki ilivyoanza..

UTALIII WA NDANI UNAVYOWEZA KUWAVUTIA WATU WENGI

Mamba mkubwa zaidi anayepatikana katika ‘hifadhi’ Kaole Mamba Ranch akiwa na umri wa miaka 30.
Na Elius Kambili, aliyekuwa Bagamoyo
UNAPOZUNGUMZIA utalii nchini, wananchi wengi wanadhani jukumu hilo hupaswa kufanywa na raia wa kigeni hasa wazungu, lakini ukweli ni kwamba utalii unaweza kufanywa hata na raia wa nchi husika kulingana na ufahamu wao wa mambo mbalimbali kuhusu faida za utalii.

Katika medani ya utalii, Tanzania imebarikiwa kuwa na wanyama na maliasili nyingi ambazo sehemu yake kubwa hazipo katika maeneo mengine duniani.

Katika sura nyingine, watu wengi hudhani kwamba Bagamoyo ni sehemu ya utalii inayohusisha mambo ya kale tu, hasa majengo ya kale yaliyokuwa yanakaliwa na wakoloni na wageni wengi waliofika huko katika miaka ya nyuma.

Katika hali halisi, mambo ni tofauti, kwani ndani ya Bagamoyo kunaweza kufanyika utalii wa aina nyingine ukiachana na ule wa mambo ya kale.

Umbali wa kilomita tano kutoka Bagamoyo mjini, inapatikana ‘hifadhi’ ndogo ya mamba iitwayo Kaole Mamba Ranch. Haikupewa jina la hifadhi kutokana na labda masharti ya sera au utaratibu mwingine husika, lakini ndani yake kuna mamba wafugwao ambao wangefaa kuwa sehemu ya hifadhi.

Sehemu hiyo inafuga mamba ambao wanaonyeshwa hatua kwa hatua kwa watalii kutoka nje ya nchi, ambapo kwa nchini kuna watu wachache sana wanaotembelea eneo hilo. Ranchi hiyo inafuga mamba zaidi ya 75, ambapo mdogo akiwa na umri wa mwaka mmoja na mkubwa ni yule mwenye miaka 30.

Kwa mujibu wa Mhifadhi ranchi hiyo, Mussa Bakari, mamba ana uwezo wa kuishi hata miaka 300 kulingana na mazingira atakayokuwapo.

“Hapa tuna mamba aina ya Nile Crocodile, hawa tunawapata kutoka sehemu mbalimbali ambapo mwengine wanazaliwa hapahapa,” anasema Mussa.

Kwa mujibu wa Mussa, mamba hao wanakula mlo mmoja tu kwa wiki kulingana na tabia yao ya kumeza milo mikubwa. Chakula kikuu wakipatacho hapo ni nyama za ng’ombe, kuku, mbuzi. n.k.

‘Hifadhi’ hiyo si kubwa sana (hasa sehemu yenye mamba) kwani mtu anaweza kutumia dakika 20 kutembelea mabanda yote yanayohifadhi wanyama hao na kupata maelezo ya tabia mbalimbali kuhusu jinsi wanavyofugwa hapo.

Kivutio kikubwa hapo ni kwamba watalii wa ndani, yaani raia wa Tanzania, hutozwa 1,000/= tu kutembelea sehemu hiyo ambayo ndani yake kuna viota vingi vya ndege wenye rangi mbalimbali zivutiazo.

Ranchi hiyo ina miaka 18 tangu ilipoanzishwa mwaka 1992, na imekuwa ikiuza nyama na ngozi ya mamba ndani na nje ya nchi.
Mamba wakiwa katika hifadhi yao.
Mamba wadogo zaidi wanaopatikana katika hapo ambao wana umri wa mwaka mmoja.
Watalii wachache wa ndani wakitazama mamba katika moja ya mabanda ya kuhifadhia wanyama hao.
Viota na ndege wakiwa katika mti ulio ndani ya kituo hicho.

KATUNI


Posted by Herman on November 16, 2010 at 8:35am 



Monday, November 15, 2010

RIPOTI KAMILI

Na Luqman Maloto, aliyekuwa Dodoma
Bunge la 2010-2015 ni la vijana, mandhari na kila kitu kinabeba tafsiri hiyo na hapa kuna ripoti kamili ya kilichochukua nafasi mjini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Bunge la 10.
Bunge.
Jicho la Ijumaa Wikienda bungeni lina tathmini ya jumla kuwa bunge jipya lina idadi kubwa ya vijana kuliko wazee, tofauti na ilivyozoeleka miaka ya nyuma.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho pekee kinachoongoza kwa kutumbukiza wazee mjengoni, ingawa vijana ni wengi zaidi, kikifuatiwa na Chama cha Wananchi (CUF).
John Mnyika, Ubungo.
Chama cha NCCR-Mageuzi, ndicho kilichotia fora zaidi kwa kuingiza wabunge wanne na kati yao robo tatu ni vijana chini ya umri wa miaka 30, isipokuwa mwana mama Agripina Zaitun Buyogera wa Kasulu Vijijini.

NCCR kimevunja rekodi ya CHADEMA katika bunge lililopita, wakati mbunge wake, Zitto Zuberi Kabwe alipoingia mjengoni akiwa na umri wa miaka 28, hivyo kuwa kijana mdogo zaidi kutoka jimboni.
Mchungaji Peter Msigwa, Iringa Mjini.
Safari hii, Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR) ndiye mbunge mdogo zaidi ambapo ameingia mjengoni akiwa na umri wa miaka 24.

JUMANNE, MPAKA ALHAMISI ILIYOPITA
Idadi ya wabunge waliowasili kwa ajili ya kujisajili ilikuwa ndogo Jumanne, siku iliyofuata (Jumatano) iliongezeka lakini walifurika Alhamisi ambapo ndiyo ilikuwa mwanzo wa utambulisho bungeni.
Catherine Magige, Viti Maalum (UVCCM- Arusha) .
Mandhari ya Jumatano yalikuwa ni yenye kuchangamka, wabunge wakipongezana kwa kufanikiwa kushinda, wengine wakirejea na wale waliofanikiwa kwa mara ya kwanza.

SLAA, MBOWE WAITEKA DOM USIKU
Msafara mkubwa wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Willibrod Slaa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe uliwasili Jumanne usiku mjini Dom na kufanya mkutano kwenye makao makuu ya chama mkoa.
David Kafulila, Kigoma Kusini.
Mkutano ulipambwa na shamrashamra, wakazi wa Dom wakimshangilia Slaa alipokuwa anawasili na hata alipoanza kuhutubia.

Hata hivyo, baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’ kuwasili kwenye mkutano huo, wananchi walipoteza umakini kwa Slaa na kuanza kumshangilia shujaa huyo wa Bongo Flava.
Zitto Kabwe, Kigoma Kaskazini.
Busara za Slaa, zilimuongoza kumwita mbele Sugu a.k.a Mr. II aweze kuwasalimia wananchi kwa uwazi na baada ya hapo mkutano ulifungwa.

SITTA AVUTA HISIA
Jumatano majira ya saa 5 asubuhi, Spika wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta aliwasili bungeni kujisajili na kuzungukwa na umati mkubwa wa watu, wengi wakiwa ni waandishi wa habari na wabunge.
Ezekia Wenje, Nyamagana.
Akiwa mwenye uchangamfu, alikuwa akiwatania wabunge hasa wale waliopita mbali naye, huku akiwakumbusha kwamba yeye ni mgombea wa uspika.

HARUFU MBAYA BUNGENI
Dalili ya hatari ndani ya CCM na bunge, zilionekana kwenye viunga vya bunge kutokana na kampeni za waziwazi ambazo zilikuwa zinaendeshwa.
Lucy Mayenga, Viti Maalum (Wanawake-Shinyanga).
Makundi ya wazi yalionekana, upande mmoja ukitaka Sitta apite, wakati mwingine ukishinikiza aenguliwe mapema.

Upande mmoja ulikuwa ukiwaomba wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM (CC), wakate jina la Sitta kwa kile walichodai kwamba matokeo ya kushuka ilichopata chama hicho katika Uchaguzi Mkuu uliopita yalisababishwa na yeye.
Halima Mdee, Kawe.
Hata hivyo, upande wa pili, walidai Sitta ndiyo sababu ya ushindi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2010, vinginevyo chama hicho kingeangushwa mwereka mkubwa.

Walidai kuwa uongozi wa Sitta ulionesha wananchi kwamba ndani ya CCM kuna watu makini walio tayari kujikosoa ndiyo maana wakakipigia kura.
Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu, Mbeya Mjini.
KIGOGO AVUJISHA SIRI YA KAMATI
Jumatano, saa saba mchana, kigogo mmoja wa chama alivujisha siri alipowasili bungeni baada ya kumnong’oneza mbunge mmoja kwamba mwaka huu spika atakuwa mwanamke.

Sababu alizotoa, ndizo zilizoonekana katika taarifa rasmi kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati siku hiyo hiyo jioni.
WAHESHIMIWA CLUB 84
Jicho la Ijumaa Wikienda lilizama ndani ya Club 84 ambayo ina jina kubwa na kujionea waheshimiwa kadhaa (majina tunayo) wakijirusha, huku wengine wakiondoka eneo hilo karibu na majogoo.

BUNGENI KIMYA
Alhamisi kwa watu wengi ilikuwa kama msiba bungeni, wakisikitikia uamuzi wa kamati, ikiwemo wafanyakazi wa bunge lakini hakukuwa na jinsi.
Kikao cha kamati ya Wabunge wa CCM, kilikaa kuchagua kati ya majina matatu, Anna Makinda, Anna Abdallah na Kate Kamba ambapo jina la Makinda liliposhinda, shamrashamra zilianza.

Wakati hali ikiwa hivyo, CHADEMA kilikuwa ‘bize’ na vikao, kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni.
Idd Azzan, Kinondoni.
DOM GESTI, HOTELI
Tathmini Dodoma, kila mtaa kuna gesti na hoteli kadhaa na kwa hesabu, bila shaka ndiyo mkoa wenye gesti na hoteli nyingi Tanzania.

MADENTI U-DOM
Wanafunzi wanaosoma Chuo Kikuu cha Dodoma (U-Dom), walionekana wakirandaranda kwenye hoteli za waheshimiwa, na walipatikana pia mitaani wakati huu wa bunge jipya.
Neema Mgaya Hamid (Viti Maalum, UVCCM-Dar)
NI MREMBO?
Bunge lililopita lilikuwa na warembo wengi lakini mwaka huu ni ‘funika bovu’.

Nani mkali ni mchuano kati ya Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Catherine Magige ‘Pamela’, Mbunge Viti Maalum CCM (Geita), Vicky Kamata ‘Madame V’ na Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee.
Vita Kawawa,
Wengine ni Mbunge wa Viti Maalum CCM (Shinyanga), Lucy Mayenga, Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA (Kigoma), Mhonga Ruhanywa, Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Neema Mgaya Hamid na Mbunge wa Viti Maalum CCM (Zanzibar), Tawhida Cassian Gallus.

HANDSOME BOYS
Ingizo jipya la wabunge vijana linafanya mchuano uwe mkali katika bunge hili.
Mnyika na David Silinde wakibadilishana mawazo.
Zitto, Mkosamali, Sugu wamo kwenye orodha, halafu wapo wengine kama Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika, Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba na Mbunge wa Mbozi Magharibi (CHADEMA), David Silinde.

Wengine ni Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA), Ezekia Wenje, Mbunge wa Ilemela (CHADEMA), Highness Kiwia, Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbless Lema na wengineo.
Sugu na Mnyika wakipata msosi.